Siku ya ijuma ya wikii hii [June 16,2017] Mji wa Ifakara ulikimbiza mwenge wa
uhuru baada ya kuupokea kutoka Wilaya Malinyi ambapo ulikimbizwa katika miradi 8 iliyopo mjini hapa huku 5 ni ya kuwekwa jiwe la msingi miwli ikiwa ya kuzinduliwa na moja ukiwa wa kuonwa .
Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa Ujenzi wa maabara shele ya sekondari kilombero kwa ajili ya masomo ya phizikia na kemia,mradi wa ‘’ NGAKAWE ‘’wenyelengo la utoaji wa elimu ya kupiga vita dawa za kulevya na vitendo vya rushwa, mradi wa Eneo lilotengwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda ,mradi wa ujenzi wa hositali ya kansa ,mradi wa mpango endelevu wa kuthibiti na kupambana na ugonjwa wa malaria, Mradi mwingine ni pamoja na kikundi cha ujasriamali, mradi wa ujenzi wa ofisi ya kata, pamoja na mradi wa Programu ya upandaji miti.
Jumla ya miradi hiyo yote mpaka kukamilika kwake ni sh. Bilioni 1.6kwa michango iliyotolewa kupitia ngavu za wananchi na Fedha iliyotolewa na serikali kuu Halmashauri ya mji kwa kushirikiana na wahisani wa mashirika mbalimbali
Katika miradi yote hiyo kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru ndug Amour H Amour amesisitiza juu ya matumizi bora ya fedha za serikali ambapo aliagiza miradi yote ilingane na thamani ya pesa iliyo tumika kuikamilisha.
Ninawapongeza sana kwa kuwa na kiwanda kikubwa na kizuri kuliko vyote katika maeneo yote ambapo mwenge umepita napia naomba ni sisitize juu ya utoaji huduma bora zenye kufuata weledi kwa wana nchi ilithamani na uzuri wa jingo hili uendane na huduma wanazo pata wananchi huku mkizingatia kuwa madaraka mliyo nayo yanatokana na uwepo wa wananchi hawa’’Aliongeza Amour.
Akiwa katika mradi wa kupambana na malaria ambao umegarimu zaidi ya sh. 1,073,562,500/= katika hospitali ya Kibaoni, Amour alisifu jitihada zilizofanywa na uwongozi Halmashauri kupitia uwongozi wa hospitali hiyo kwa kugawa bima ya afya kwa wazee wasio jiweza na vyandarua kwa wajawazito kwa kazi nzuri ya kuhakikisha wananchi wanapatiw huduma nzuri za afya nakuwa taka wananchi kujali afya zao.
Mara baada ya kumaliza mbio zake katika Halmashauri ya mji Ifakara ,mwenge wa uhuru ulikabidhiwa katika wilaya ya kilombero mkoa wa Morogoro na makabidhiano hayo kufanyika mjini Ruwaha siku ya juma mosi june 17,2017.
Mwenge wa uhuru kwa mwaka 2017umebeba ujumbe unaosema ’’Shiriki kukuza uchimi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu.
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Simu ya Mkononi: 0738 223 543
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa