• Mawasiliano Yetu |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ifakara Town Council
Ifakara Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Ifakara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wasifu wa Halmashauri
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Ujenzi
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu & Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo,Ushirika & Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Manunuzi & Ugavi
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
  • Huduma
    • Ukodishaji wa Mitambo
    • Upimaji,Usanifu wa Viwanja,Majengo &Mashamba
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za kudumu
    • Kata
      • Mbasa
      • Katindiuka
      • Mlabani
      • Lumemo
      • Kibaoni
      • Viwanja sitini
      • Ifakara
      • Michenga
      • Lipangalala
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • CHF iliyoboreshwa
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Kanuni
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Mifumo

CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO (SUA) KUWEZESHA VIJANA KUONGEZA UZALISHAJI NA MNYORORO WA THAMANI WA MAZAO - HALMASHAURI YA MJI IFAKARA

Posted on: October 6th, 2025

CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO (SUA) KUWEZESHA VIJANA KUONGEZA UZALISHAJI NA MNYORORO WA THAMANI WA MAZAO KATIKA HALMASHAURI YA MJI IFAKARA

Chuo Kikuu cha Sokoine cha  Kilimo  (SUA) kimetambulisha Rasmi Mradi wa TAGDev 2.0 AGRIFOSE -RIH, unaotekelezwa chini ya RUFORUM kwa ufadhili wa Mastercard Foundation kwa Vikundi 18 vya Vijana katika Halmashauri ya Mji Ifakara, Mkoani Morogoro.

Utambulisho huo umefanyika Leo Jumatatu Oktoba 6.2025 umehusisha Vikundi vya Vijana kutoka Kata nne za Kiberege, Katindiuka, Kisawasawa na Signal ambapo Mradi huo unalenga kuongeza uzalishaji na Mnyororo wa thamani wa mazao ya Mpunga na mbogamboga ukiwapa kipaumbele Vijana wakike wanaounda zaidi ya asilimia 70 ya Walengwa.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo , Mratibu wa Mradi kutoka SUA , Dkt. Hamisi Tindwa alisema Mradi huo utawajengea Vijana uwezo wa kuendesha biashara katika Sekta ya Kilimo badala ya kubaki katika uzalishaji pekee.

"Mradi huu utamwezesha Kijana sio tu kuzalisha , bali pia kuchakata mazao na kushiriki katika biashara. Baada ya miaka mitano ya utekelezaji wake, kuanzia Januari 2025 hadi Desemba 2029 tutapima mafanikio kwa idadi ya biashara mpya zitakazozaliwa kupitia Vijana hawa ". AlisemA Dkt. Tindwa

kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Wakili Dunstan Kyobya ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika warsha hiyo aliwapongeza Vijana waliochaguliwa kushiriki  katika Mafunzo  hayo, akiwataka kutumia maarifa watakayopata kuongeza ubunifu, matumizi ya teknolojia na masoko ya bidhaa zao.

"Nataraji kuona Vijana hawa wakibadilika na kutumia teknolojia za Kisasa katika uzalishaji na biashara ya mazao yao. Huu ni mwanzao wa mabadiliko makubwa katika uchumi wa Vijana wetu" . alisema Mhe. Kyobya

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Bw. Said Majaliwa aliishukuru SUA kupitia Mradi wa RUFORUM kwa kuona umuhimu wa kuwawezesha Vijana katika Sekta ya Kilimo, akibainisha kuwa elimu hiyo italeta tija kubwa kwa jamii.

Mmoja wa Wasiriki wa Mafunzo hayo , Bi. Consolata Fabian kutoka Kikundi cha Promise cha Kisawasawa , alitoa shukrani kwa SUA kwa ujuo wa Mradi huo, akisema utawasaidia kupata maarifa mapya na kuongeza kipato kupitia shughuli za Kilimo Biashara.

Mradi wa TAGDev 2.0 AGRIFOSE -RIH ni sehemu ya Programu ya RUFORUM inayotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA), Chuo cha Nelson Mandela (ARUSHA), Chuo Kikuu cha Dar es Salaama (UDSM), na Jukwaa la Vyuo Vikuu Afrika (RUFORUM) kwa ufadhili wa Mastercard Foundation.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA KUPIGA KURA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA KITUO TOFAUTI NA KITUO ALICHOJIANDIKISHA September 18, 2025
  • TANGAZO LA ULIPAJI WA ADA NA USHURU KWA WANANCHI, WAFANYABIASHARA NA TAASISI MBALIMBALI IFAKARA MJI October 03, 2025
  • Ona yote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YAKABIDHI VITI NA MEZA 100 SHULE YA SEKONDARI MAHUTANGA

    October 08, 2025
  • CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO (SUA) KUWEZESHA VIJANA KUONGEZA UZALISHAJI NA MNYORORO WA THAMANI WA MAZAO - HALMASHAURI YA MJI IFAKARA

    October 06, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YA KILOMBERO (KU) YAMPONGEZA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MJI IFAKARA BI . PILLY KITWANA KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

    October 03, 2025
  • WAZEE WATAKIWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI NCHINI

    October 01, 2025
  • Ona yote

Video

Shangwe la Mkesha wa Mwenge 2025 Uwanja wa CCM Mkamba Kidatu Msanii wa Muziki MC Hamza akiimba na wanaIfakara, Tarehe 17-04-2025.
More Videos

Kurasa za Haraka

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024
  • Ramani ya halmashauri ya mji wa Ifakara
  • BOFYA HAPA KUOMBA KITAMBULISHO CHA WAJASILIAMALI WADOGO
  • CHF

Kurasa Mfanano

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya utumishi wa uma
  • Tovuti ya mkoa wa Morogoro
  • Tovuti ya Ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Mawasiliano Yetu

    Kibaoni - Bomani

    Sanduku la Barua: 433 Ifakara

    Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212

    Simu ya Mkononi: -

    Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Uhifadhi
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa