• Mawasiliano Yetu |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ifakara Town Council
Ifakara Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Ifakara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wasifu wa Halmashauri
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Ujenzi
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu & Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo,Ushirika & Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Manunuzi & Ugavi
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
  • Huduma
    • Ukodishaji wa Mitambo
    • Upimaji,Usanifu wa Viwanja,Majengo &Mashamba
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za kudumu
    • Kata
      • Mbasa
      • Katindiuka
      • Mlabani
      • Lumemo
      • Kibaoni
      • Viwanja sitini
      • Ifakara
      • Michenga
      • Lipangalala
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • CHF iliyoboreshwa
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Kanuni
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Mifumo

BAJAJI,BODABODA KUANZA KUSAJILIWA NA KUKATIWA LESENI ZA USAFIRISHAJI ABIRIA IFAKARA,MKURUGENZI AAHIDI KUSIMAMIA UUNDAJI WA UMOJA WAO

Posted on: October 3rd, 2017

Mamlaka ya Udhibiti   wa Usafiri wa abiria na mizigo wa  nchikavu na Majini ( SUMATRA) imesema ipo mbioni kuzikatia Leseni na kuzisajili  Pikipiki zote za magurudumu matatu na mawili zinazotoa huduma ya kusafirisha abiria katika Mji wa Ifakara kwa Ushirikiano na Halmashauri ya Mji Ifakara na kwamba hatua hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Usafirishaji na kanuni zake zilizoanza kutumika mwaka 2011.

Hayo yamethibitika  katika kikao  cha pamoja kati ya Wamiliki na Madereva wa Bodaboda na Pikipiki, SUMATRA  na  Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani wilaya ya Kilombero kilichoitishwa na  Halmashauri ya Mji Ifakara kwa lengo la kuwapatia elimu Wamiliki na Madereva wa Vyombo hivyo vya usafiri kabla ya kuanza kwa zoezi la kuwasajili na kuwakatia Leseni  hizo.

 Afisa  Mfawidhi   wa SUMATRA Mkoa wa Morogoro ndugu Joseph Burongo ameeleza kuwa kwa mujibu wa Sheria na kanuni  ya Usafirishaji, Pikipiki zote za magurudumu matatu zinazotoa huduma ya kusafirisha abiria zinapaswa kusajiliwa na kupatiwa Leseni kwani Sheria hiyo na kanuni zake zilianza kutumika miaka saba iliyopita na kwamba SUMATRA imeingia makubaliano na Halmashauri zote nchini na kukasimu madaraka yake ya kuvikatia Leseni vyombo hivyo vya usafiri vinavyohudumia  abiria kwa Halmashauri kupitia kitengo cha Biashara.

Afisa Mfawidhi huyo wa SUMATRA alifafanua kuwa kila chombo kinachotoa huduma ya kusafirisha abiria kina kiwango cha ada na leseni yake na kueleza kuwa kwa bodaboda ni Tsh.22,000/ wakati bajaji ni Tsh 32,000/ kwa mwaka mzima na kueleza kuwa ili mmiliki aweze kupatiwa Leseni hiyo atapaswa kufika Halmashauri ya Mji kitengo cha biashara, akiwa na nakala ya kadi ya chombo husika kwa wale ambao kadi hizo zimeandikwa majina yao na kwa wale ambao hawajahamisha umiliki watapaswa kuwasilisha nakala ya kadi iliyopo pamoja na nakala ya kitambulisho kimojawapo kati ya leseni ya udereva,kitambulisho cha Mpiga kura ,kitambulisho  cha Uraia au Hati ya kusafiria na kwamba ada ya Leseni ya usafirishaji itaanza kutozwa katika kipindi husika cha usajili hata kama utekelezaji wa Sheria hiyo ulianza miaka saba iliyopita na kwamba hakutokuwa na Bajaji au Bodaboda itakayoruhusiwa kusafirisha abiria bila kuwa na Leseni ya Usafirishaji mara zoezi la usajili litakapoanza Ifakara.

Kwa upande wake Jeshi la Polisi kupitia  kikosi cha Usalama barabarani wamewataka Waendesha Bodaboda hao  kutii Sheria  bila shuruti kwa kufuata Sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kusajili Vyombo vyao vya usafiri pamoja na vijiwe vyao kupitia Halmashauri kwa ajili ya kuwatambua Watoa huduma  wote,kulinda usalama wao na usalama wa abiria wanaowaendesha

“Tunaachana na utamaduni wa kufanya kazi hii kwa mazoea na kuanza kuifanya kibiashara kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa, ni kweli tumechelewa lakini ni lazima tufanye kwa mujibu wa Sheria ,mnapaswa kulinda Usalama wenu na abiria wenu ili shughuli hii iendelee kuwaingizia kipato bila bugudha.Sisi tunasimamia Sheria  hivyo baada ya zoezi la usajili hakuna bajaji wala bodaboda itakayobeba abiria bila kuwa na Leseni ya usafirishaji.”Alisema Leus Yazidi Msimamizi wa nidhamu na Mtoa   Elimu ya Barabarani  Jeshi la Polisi Wilaya ya Kilombero.

Naye Kaimu Mkuu wa Usalama Barabarani Wilaya ya Kilombero Inspekta Nkilijiwa Lazaro, aliwataka Waendesha bajaji na bodaboda hao kuanza kujiandaa mapema ili kutii utaratibu huo mara usajili utakapotangazwa  na Halmashauri  kwani suala hilo ni la kisheria na hivyo halina mjadala na hata maeneo mengine utekelezaji wa Sheria hiyo umeanza muda mrefu na kuongeza kuwa angalau Watu wa Ifakara wamepata fursa ya kuelimishwa kabla ya kuanza utekelezaji, hivyo ni vyema wakatii maelekezo wanayopewa kwani utekelezaji wa Sheria hiyo ungeweza kuanza hata bila ya kutolewa Elimu kwa kuwa kutokujua Sheria sio kinga bali ni kosa pia.

Awali akifungua mkutano huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara ndugu Francis Ndulane alisema kuwa wao kama Halmashauri ambao ndiyo wamekasimiwa madaraka ya utoaji wa Leseni hizo na SUMATRA wameona ni vyema kuwakutanisha Wadau wote na kuwapatia Elimu hiyo ili kuwa na uelewa wa pamoja ambao utarahisisha   zoezi hilo ambalo litaanza hivi karibuni

Katika hatua nyingine Mkurugenzi  Ndulane, aliahidi kusimamia Utaratibu wa kuunda  Umoja wa Waendesha Bajaji na Pikipiki wote katika Mji wa Ifakara (TAMOSA) ili nao waweze kunufaika na fursa za mitaji zinazotolewa kupitia umoja huo na Wadau wa maendeleo ikiwemo mikopo ya fedha,pikipiki na bajaji na hatimaye Waendesha Bodaboda na Bajaji  wa Ifakara waweze kumiliki biashara zao wao wenyewe, kuwa na vyanzo vya mapato zaidi ya kimoja, kukuza uchumi wa familia zao na kuchangia maendeleo ya Halmashauri ya Mji Ifakara na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA MANG'ULA February 07, 2025
  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA IFAKARA February 07, 2025
  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA KIDATU February 07, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE HALMASHAURI YA MJI IFAKARA November 01, 2022
  • Ona yote

Habari Mpya

  • WATUMISHI HALMASHAURI YA MJI IFAKARA NA HALMASHAURI YA WILAYA MLIMBA WAJENGEWA UWEZO JUU YA UTEKELEZAJI WA MFUMO WA USIMAMIZI WA UTENDAJI KAZI KATIKA UTUMISHI WA UMMA (e -UTENDAJI).

    June 26, 2025
  • WATUMISHI HALMASHAURI YA MJI IFAKARA NA HALAMSAHURI YA WILAYA MLIMBA WAJENGEWA UWEZO JUU YA UTEKELEZAJI WA MFUMO WA USIMAMIZI WA UTENDAJI KAZI KATIKA UTUMISHI WA UMMA (e -UTENDAJI).

    June 26, 2025
  • WAKULIMA WA HALMASHAURI YA MJI IFAKARA WAHAKIKISHIWA KUENDELEA KUZALISHA MAZAO NA KUPATA FAIDA ZAIDI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI

    June 11, 2025
  • VIZIMBA MAALUM VYA KUTUPA MAKOPO YA VIUWATILIFU VYATAKIWA KUJENGWA KATIKA KATA ZA HALMASHAURI YA MJI IFAKARA.

    June 05, 2025
  • Ona yote

Video

Shangwe la Mkesha wa Mwenge 2025 Uwanja wa CCM Mkamba Kidatu Msanii wa Muziki MC Hamza akiimba na wanaIfakara, Tarehe 17-04-2025.
More Videos

Kurasa za Haraka

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024
  • Ramani ya halmashauri ya mji wa Ifakara
  • BOFYA HAPA KUOMBA KITAMBULISHO CHA WAJASILIAMALI WADOGO
  • CHF

Kurasa Mfanano

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya utumishi wa uma
  • Tovuti ya mkoa wa Morogoro
  • Tovuti ya Ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Mawasiliano Yetu

    Kibaoni - Bomani

    Sanduku la Barua: 433 Ifakara

    Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212

    Simu ya Mkononi: -

    Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Uhifadhi
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa