Na: Nuru Mangalili – Ifakara Tc , Habari
Wataalam Wilaya ya Kilombero wapatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya Utekelezaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Utendaji kazi katika Utumishi wa UMMA (e - Utendaji) leo Alhamisi tarehe 26 Juni 2025 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mlimba uliopo Ifakara Mji. Wawezeshaji katika Kikao hicho ni Bi. Shomi Jonas na Bw. Mutani Josephat Manyama kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Aidha, Mafunzo hayo yamehudhuriwa na Wakurugenzi wa Halmashauri za Mji Ifakara na Halmashauri ya Wilaya Mlimba, Wakuu wa Idara, Vitengo, na Sehemu. Wafawidhi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya, Maafisa Elimu Kata na Watendaji wa Kata wa Halmashauri zote mbili ambazo ni Halmashauri ya Mji Ifakara na Halmashauri ya Wilaya Mlimba.
Akizungumza wakati akihitimisha Mafunzo hayo Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero Ndugu Abraham Mwaikwila aliwashukuru Wawezeshaji hao kwa kuwasaidia watumishi kuendelea kuuelewa Mfumo huo wa kupima utendaji kazi na shughuli zinazofanyika kila siku za Mtumishi kwa njia ya Mtandao.
“Kadri tunavyozidi kuutumia Mfumo huu ndivyo tunavyozidi kuuelewa zaidi, Kikao hiki kimeendelea kutusaidia zaidi namna ya kutumia mfumo huu Vizuri tunawashukuru kwa mafunzo”. Alieleza Ndugu, Mwaikwila.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Bw. Thomas Luambano alitoa Rai kwa kila Mtumishi kuhakikisha anafuatilia Mpango Mkakati na Malengo yake katika Mfumo huo wa Utendaji Kazi kwa Watumishi ili waweze kutumia Mfumo huo kwa wepesi
Wakati huohuo Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Bw. Rashidi Semngoya aliendelea kusisitiza watumishi kujaza majukumu yao ya kila siku katika Mfumo huo
”Mfumo huo utaamua utendaji kazi wa Mtumishi kama Mtu hatajaza majukumu yake ya kila siku mfumo unaweza kusababisha watumishi kutokwenda likizo, kukosa Mshahara, kutokupanda Vyeo, kushindwa kupata Mkopo n.k hivyo kila mtumishi ahakikishe anajaza na kutuma kwa Mkuu wake wa Idara, Kitengo na Sehemu na sisi Viongozi tunatakiwa tuhakikishe tuna idhinisha kazi za Watumishi na kuwafanyia tathmini .”. Alisisitiza Bw. Semgoya
Aidha, mmoja kati ya Wakufunzi hao kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Mutani Manyama alisisitiza Viongozi kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kuwafanyia tahmini watumishi kwenye Mfumo kwani wasipofanya hivyo Serikali itakosa taarifa za Mtumishi kwenye Mfumo .
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Simu ya Mkononi: -
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa