Wakulima wa Mazao katika Halmashauri ya Mji Ifakara wamehakikishiwa kuendelea kuzalisha Mazao yao na kupata faida zaidi kwa kupitia mfumo wa Stakabadhi za Ghala.Hayo yamesemwa tarehe 11 Juni 2025 wakati wa Kikao cha Kujadili namna ya kusimamia Utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwa Wakulima wa Mazao mbalimbali hususani katika kuelekea Msimu wa Ufuta, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero.
Kikao hicho kiliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Wakili Dunstan Dominick Kyobya ambapo kilishirikisha Bodi ya Usimamzii wa Stakabadhi za Ghala kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, Viongozi wa Mabenki, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Bw. Said Majaliwa na Wataalamu kutoka Mkoa wa Morogoro na Halmashauri ya Mji Ifakara.
Aidha Mkurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala Ndugu , Asangye Bangu alisema Mfumo wa Stakabadhi za Ghala upo kuhakikisha wakulima wa Mazao mbalimbali kama Ufuta, Kokoa n.k wanapata bei za ushindani zilizoko Sokoni.
"Mkoa wa Morogoro umefanya jitihada kubwa kuhakikisha Mfumo wa Stakabadhi unafanya vizuri hususani hapa Halmashauri ya Mji Ifakara, ambapo wakulima wataendelea kuzalisha na kupata faida nyingi". Alieleza Ndugu Asangye Bangu
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilombero Ndugu Abraham Mwaikwila alisema kuwa suala la Stakabadhi Ghalani linatakiwa kuendele a kuelimishwa zaidi kwa Wananchi na Wakulima ndani ya Wilaya ya Kilombero ili iweze kuwasaidia Wananchi kuondokana na umaskini kwa wakulima na kupata faida zaidi
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Simu ya Mkononi: -
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa