• Mawasiliano Yetu |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ifakara Town Council
Ifakara Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Ifakara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wasifu wa Halmashauri
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Ujenzi
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu & Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo,Ushirika & Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Manunuzi & Ugavi
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
  • Huduma
    • Ukodishaji wa Mitambo
    • Upimaji,Usanifu wa Viwanja,Majengo &Mashamba
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za kudumu
    • Kata
      • Mbasa
      • Katindiuka
      • Mlabani
      • Lumemo
      • Kibaoni
      • Viwanja sitini
      • Ifakara
      • Michenga
      • Lipangalala
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • CHF iliyoboreshwa
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Kanuni
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Mifumo

UJENZI WA SOKO JIPYA LA KIBEREGE KUKAMILIKA HIVI KARIBUNI

Posted on: January 12th, 2025

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Ifakara Mhe. Kassim Faya Nakapala amesema Ujenzi wa Soko la Kiberege katika  Kata ya Kiberege Halmashauri ya Mji Ifakara unatarajiwa kukamilika hivi Karibuni kutokana na  mradi huo kuendelea kutengewa bajeti ili kukamilisha ujenzi wake kwa Mwaka  Mpya wa Fedha  2025/2026.


Hayo ameyasema  Jumamosi tarehe 11 Januari 2025 wakati  akijibu swali lililoulizwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) Wilaya ya Kilombero  Ndugu, Mohammed Msuya kuhusu maendeleo ya Mradi huo wakati wa  Mkutano Mkuu wa Halmashauri  Kuu ya CCM Wilaya ya Kilombero kupitia Utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi.


Akijibu swali hilo Mhe. Nakapala alisema mpka sasa  Mradi huo wa Soko la Kiberege tayari umetengewa pesa  ya kukamilisha ujenzi wake katika bajeti ya mwaka 2025/ 2026 ambapo pesa hizo ni za Mapato ya Ndani ya Halmashauri na Mpaka kukamilika kwake Mradi utagharimu kiasi cha Shilingi Milioni 34,000,000.


 " Ili miradi ikamilike Halmashauri inatakiwa kuongeza kasi ya Ukusanyaji wa Mapato kwani Mradi huo ni miongoni  mwa miradi inayotegemea mapato ya ndani ili iweze kukamika ". Alisema Mhe. Nakapala


Sambamba na hilo , Mhe. Nakapala alieleza kuwa mpaka sasa Halmashauri imekusanya  kiasi cha Shilingi  2, 874,097,273 sawa na asilimia 44 ya Makusanyo ya Fedha za Mapato yote ya ndani ambayo lengo lake la Makusanyo kwa bajeti ya mwaka wa Fedha 2024 /2025 ni Sh. 6, 587,395,510.


Aidha Muheshimiwa Nakapala alieleza baadhi ya Changamoto zinazokabili Halmashauri katika ukusanyaji wa Mapato na kueleza kuwa tayari Halmashauri imeshaweka mikakati ya kuongeza wigo wa Ukusanyaji wa Mapato na kuahidi kufikia lengo la asilimia 100  ya Ukusanyaji wa Mapato ifikapo mwisho wa mwaka wa Fedha 2024/2025.









Matangazo

  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA MANG'ULA February 07, 2025
  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA IFAKARA February 07, 2025
  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA KIDATU February 07, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE HALMASHAURI YA MJI IFAKARA November 01, 2022
  • Ona yote

Habari Mpya

  • MKUTANO WA TRA NA WAFANYABIASHARA WILAYA YA KILOMBERO

    March 05, 2025
  • HAMASA YATOLEWA KWA JAMII YA WAFUGAJI KUSHIRIKI MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI PAMOJA NA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA IFAKARA TC

    February 27, 2025
  • MAFUNZO KWA WATENDAJI NGAZI YA JIMBO JUU YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 22, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA KILOMBERO KUANZA TAREHE 1 MACHI, 2025 HADI TAREHE 7 MACHI 2025

    February 24, 2025
  • Ona yote

Video

Shangwe la Mkesha wa Mwenge 2025 Uwanja wa CCM Mkamba Kidatu Msanii wa Muziki MC Hamza akiimba na wanaIfakara, Tarehe 17-04-2025.
More Videos

Kurasa za Haraka

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024
  • Ramani ya halmashauri ya mji wa Ifakara
  • BOFYA HAPA KUOMBA KITAMBULISHO CHA WAJASILIAMALI WADOGO
  • CHF

Kurasa Mfanano

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya utumishi wa uma
  • Tovuti ya mkoa wa Morogoro
  • Tovuti ya Ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Mawasiliano Yetu

    Kibaoni - Bomani

    Sanduku la Barua: 433 Ifakara

    Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212

    Simu ya Mkononi: -

    Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Uhifadhi
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa