Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Bi. Pilly Kitwana amewahimiza Wananchi wa Halmashauri ya Mji Ifakara na maeneo ya jirani kujitokeza kwa wingi kupata huduma za Matibabu ya Kibingwa kutoka kwa Madaktari Bingwa waliotoka nchini Italia wakishirikiana na Madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mtakatifu Fransisko - Ifakara kwaajili ya kutoa huduma za Matibabu ya Upimaji wa Magonjwa ya Masikio , Pua na Koo . Mdomo sungura, Matende na mabusha , vidonda n.k
Hayo ameyasema leo tarehe 28 Mei ,2025 wakati akizindua huduma za Matibabu ya Kibingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mtakatifu Fransisko zinazotolewa na Madaktari hao waliotoka nchini Italia kwa kushirikiana na Madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mtakatifu Fransisko Ifakara.
Aidha alimshukuru Mhe.Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha mahusiano kati ya Taasisi za Dini na Serikali ambayo yanapelekea kuboresha utolewaji wa huduma kwa jamii.
Wakati huohuo Mkurugenzi wa Tiba Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mtakatifu Fransisko Ifakara Fr. Dkt . Winifridi Gingo alisema Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa ya Mtakatifu Fransisko hupokea Madaktari hao kila mwaka kwa ajili ya kutoa huduma za Kibingwa kwa Wagonjwa hao ambapo mara baada ya kumaliza huwaachia ujuzi , uzoefu na vifaa Madaktari Bingwa wa Hospitali hiyo.
" Huduma hizi zimeanza kuanzia leo tarehe 28 /5/2025 Hadi tarehe 11/6/2025 na uchunguzi wa magonjwa haya ni bure na Matibabu yake yanafanyika kwa punguzo la bei" . Alisema Fr. Dkt. Gingo
Kwa upande wake Kiongozi wa Madaktari Bingwa kutoka Bologna - Italy Dkt. Actovia Vichi alishukuru kwa Mapokezi mazuri kwa Ofisi ya Mkurugenzi kwa kushirikiana na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mtakatifu Fransisko na kuahidi kuwahudumia vizuri kwa Wagonjwa wote watakaofika hapo Kupata Matibabu.
Huduma hizo zinatolewa kwa Kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mtakatifu Fransisko -Ifakara.
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Simu ya Mkononi: -
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa