• Mawasiliano Yetu |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ifakara Town Council
Ifakara Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Ifakara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wasifu wa Halmashauri
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Ujenzi
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu & Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo,Ushirika & Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Manunuzi & Ugavi
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
  • Huduma
    • Ukodishaji wa Mitambo
    • Upimaji,Usanifu wa Viwanja,Majengo &Mashamba
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za kudumu
    • Kata
      • Mbasa
      • Katindiuka
      • Mlabani
      • Lumemo
      • Kibaoni
      • Viwanja sitini
      • Ifakara
      • Michenga
      • Lipangalala
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • CHF iliyoboreshwa
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Kanuni
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Mifumo

KV -HELP YAGAWA KUKU 100 KWA WALENGWA WA KONGA ILI KUWABORESHEA LISHE NA KIPATO

Posted on: September 22nd, 2025

KV-HELP YAGAWA KUKU 100 KWA WALENGWA WA KONGA ILI KUWABORESHEA LISHE  NA KIPATO


Katika jitihada za kuboresha lishe na kipato kwa jamii watu wa ( KONGA)Wamekuwa wanufaika wa awamu ya kwanza kutoka  Shirika la Kilombero Valley Health and Livelihood Promotion (KV-HELP) limegawa kuku 100 kwa walengwa   20 wanaohudhuria kliniki ya magonjwa sugu katika Halmashauri ya Mji Ifakara kupitia Mradi wa Health Chicken unaotekelezwa na Shirika la KV- HELP , Halmashauri ya Mji Ifakara na Chuo Kikuu cha Tiba cha Mtakatifu  Francis ( SFUCHAS) ,ikiwa ni sehemu ya kuboresha maisha na lishe kwa walengwa hao.


Tukio hilo limefanyika tarehe 22 Septemba 2025 katika Ofisi za Shirika hilo lililopo Kapolo Ifakara.


Mgeni Rasmi katika tukio hilo alikuwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara, Bw. Saidi Majaliwa, ambaye alipongeza hatua hiyo kama mfano bora wa ushirikiano kati ya serikali na taasisi zisizo za kiserikali katika kuinua maisha ya wananchi.




“Tunaishukuru KV-HELP kwa kuwa karibu na jamii, na kwa kuona mbali kwa kutoa msaada unaokwenda zaidi ya matibabu. Kuku hawa wanaweza kubadili maisha ya walengwa Hawa kwa kuwapatia lishe bora na fursa ya kujiongezea kipato,” alisema Bw. Majaliwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa KV-HELP, Bw. Iddy Mayumana, alisema kuwa mpango huo ni sehemu ya mkakati wa shirika kusaidia walengwa wanaoishi na magonjwa sugu kama vile kisukari, shinikizo la damu, na VVU  kwa njia endelevu.


“Watu wengi wanaoishi na magonjwa ya muda mrefu hukumbwa na changamoto ya lishe duni na hali ngumu ya kiuchumi. Tunatumia mbinu kama ufugaji wa kuku kuwasaidia kujenga uwezo wa kujitegemea,” alieleza Bw. Mayumana.


Walengwa waliopokea kuku hao walielezea furaha yao na kuahidi kutumia vizuri fursa hiyo. Wengi walisema kuwa msaada huo ni mwanzo wa kujikomboa kiuchumi na kuboresha afya zao kwa kula lishe bora inayopatikana kutoka kwa kuku, ikiwemo mayai na nyama.


Kwa mujibu wa KV-HELP, zoezi hilo ni sehemu ya mpango mpana wa shirika hilo wa kuimarisha afya na maisha ya watu walioko katika mazingira hatarishi kupitia miradi ya kijamii inayochangia afya na uchumi wa familia.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA KUPIGA KURA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA KITUO TOFAUTI NA KITUO ALICHOJIANDIKISHA September 18, 2025
  • TANGAZO LA ULIPAJI WA ADA NA USHURU KWA WANANCHI, WAFANYABIASHARA NA TAASISI MBALIMBALI IFAKARA MJI October 03, 2025
  • Ona yote

Habari Mpya

  • BENKI YA CRDB YAKABIDHI VITI NA MEZA 100 SHULE YA SEKONDARI MAHUTANGA

    October 08, 2025
  • CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO (SUA) KUWEZESHA VIJANA KUONGEZA UZALISHAJI NA MNYORORO WA THAMANI WA MAZAO - HALMASHAURI YA MJI IFAKARA

    October 06, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA WILAYA YA KILOMBERO (KU) YAMPONGEZA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MJI IFAKARA BI . PILLY KITWANA KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

    October 03, 2025
  • WAZEE WATAKIWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI NCHINI

    October 01, 2025
  • Ona yote

Video

Shangwe la Mkesha wa Mwenge 2025 Uwanja wa CCM Mkamba Kidatu Msanii wa Muziki MC Hamza akiimba na wanaIfakara, Tarehe 17-04-2025.
More Videos

Kurasa za Haraka

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024
  • Ramani ya halmashauri ya mji wa Ifakara
  • BOFYA HAPA KUOMBA KITAMBULISHO CHA WAJASILIAMALI WADOGO
  • CHF

Kurasa Mfanano

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya utumishi wa uma
  • Tovuti ya mkoa wa Morogoro
  • Tovuti ya Ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Mawasiliano Yetu

    Kibaoni - Bomani

    Sanduku la Barua: 433 Ifakara

    Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212

    Simu ya Mkononi: -

    Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Uhifadhi
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa