• Mawasiliano Yetu |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Ifakara Town Council
Ifakara Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Ifakara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Wasifu wa Halmashauri
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Ujenzi
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu & Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo,Ushirika & Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Manunuzi & Ugavi
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Mkaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
  • Huduma
    • Ukodishaji wa Mitambo
    • Upimaji,Usanifu wa Viwanja,Majengo &Mashamba
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
    • Ratiba za kudumu
    • Kata
      • Mbasa
      • Katindiuka
      • Mlabani
      • Lumemo
      • Kibaoni
      • Viwanja sitini
      • Ifakara
      • Michenga
      • Lipangalala
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • CHF iliyoboreshwa
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Kanuni
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Mifumo

HALMASHAURI YA MJI IFAKARA IMEPOKEA TAARIFA YA MRADI WA KAZIAFYA KUTOKA TAASISI YA AFYA IFAKARA (IHI)

Posted on: January 30th, 2025

Mradi huo ulitekelezwa  katika Shule nne za Halmashauri ya Mji Ifakara ambazo ni Miembeni, Katindiuka , Kining'ina na Kibaoni ambapo ulianza kutekelezwa mwaka 2018 hadi 2022 na Taasisi ya Afya Ifakara -( IHI)  kwa kushirikiana na Wafadhili kutoka Uswizi ( Swiss Tropical and Public Health Institute).



Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa taarifa hiyo Jumatano tarehe 29 /1/2025 , Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Dkt. Yuda Mgeni aliipongeza Taasisi hiyo kwa taarifa hiyo  kwani itasaidia  jamii  katika kuhakikisha watoto wanakua katika Mazingira mazuri ya kusoma na afya bora .


" Niwapongeze kwa kazi nzuri ya utafiti ambapo matokeo utafiti huu yatasaidia Halmashauri katika kuboresha elimu na ufaulu mashuleni kwa kuhimiza mazoezi kwa wanafunzi na kuhimiza wazazi kuhusu umuhimu wa  chakula kwa wanafunzi mashuleni ". Alisema Dkt. Yuda


Aidha , Mradi huo ulitekelezwa katika nchi tatu za  Afrika Kusini, Ivory Cost na Tanzania - Wilaya ya Kilombero lengo ikiwa ni kuchunguza umuhimu wa Mazoezi ya Viungo na Virutubisho vya ziada katika ukuaji na Maendeleo ya watoto walioko mashuleni .


Mmoja wa Wanasayansi Watafiti wa Taasisi ya Afya Ifakara (IHI) Bi. Eliahika Minja alisema katika Utafiti huo walibaini mambo mbalimbali ikiwemo watoto wengi kutokupata mlo kamili kwa kuzingatia makundi ya chakula au kupata mlo mmoja hali inayochangia udumavu na kuwa na uwezo mdogo wa kufikiri au kushindwa kushiriki Michezo au mazoezi ya viungo, hivyo alisisitiza Elimu izidi kutolewa kwa  jamii kuzingatia kuwapa watoto chakula hasa kwa makundi yote ya chakula ili kuongeza uwezo wa kusoma  wawapo mashuleni na kusisitiza vipindi vya michezo vihusishe wanafunzi kufanya mazoezi na kucheza Michezo mbalimbali.


Mradi huu ulihusisha jumla ya wanafunzi 1,055 kutoka shule hizo ambapo wasichana 543 na wavulana 494 .

Matangazo

  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA MANG'ULA February 07, 2025
  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA IFAKARA February 07, 2025
  • KUITWA USAILI BVR TARAFA YA KIDATU February 07, 2025
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE HALMASHAURI YA MJI IFAKARA November 01, 2022
  • Ona yote

Habari Mpya

  • MKUTANO WA TRA NA WAFANYABIASHARA WILAYA YA KILOMBERO

    March 05, 2025
  • HAMASA YATOLEWA KWA JAMII YA WAFUGAJI KUSHIRIKI MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI PAMOJA NA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA IFAKARA TC

    February 27, 2025
  • MAFUNZO KWA WATENDAJI NGAZI YA JIMBO JUU YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    February 22, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JIMBO LA KILOMBERO KUANZA TAREHE 1 MACHI, 2025 HADI TAREHE 7 MACHI 2025

    February 24, 2025
  • Ona yote

Video

Shangwe la Mkesha wa Mwenge 2025 Uwanja wa CCM Mkamba Kidatu Msanii wa Muziki MC Hamza akiimba na wanaIfakara, Tarehe 17-04-2025.
More Videos

Kurasa za Haraka

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024
  • Ramani ya halmashauri ya mji wa Ifakara
  • BOFYA HAPA KUOMBA KITAMBULISHO CHA WAJASILIAMALI WADOGO
  • CHF

Kurasa Mfanano

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya utumishi wa uma
  • Tovuti ya mkoa wa Morogoro
  • Tovuti ya Ajira Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Mawasiliano Yetu

    Kibaoni - Bomani

    Sanduku la Barua: 433 Ifakara

    Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212

    Simu ya Mkononi: -

    Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Uhifadhi
    • Kanusho
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa