Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Wakili Dunstan Kyobya na Menejimenti ya Halmashauri ya Mji Ifakara ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Dkt. Yuda Mgeni Julai 9 , 2025 wametembelea Masoko ya Wafanyabiashara na Samaki katika Halmashauri ya Mji Ifakara katika Eneo la Stendi ya Kibaoni na Soko la Kariakoo lililopo Mtaa wa Mhola Kata ya Viwanja Sitini.
Aidha Wafanyabiashara hao walipata nafasi ya kuelezea kero na changamoto wanazokutana nazo katika Masoko hayo ambayo huanza kazi kila siku saa 9 Alasiri mpaka saa 2 Usiku.
Mkuu wa Wilaya , Kaimu Mkurugenzi na Menejimenti ya Halmashauri ya Mji Ifakara walizipokea changamoto hizo na kuzifanyia kazi.
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Simu ya Mkononi: -
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa