Samia Day Ilivyoadhimishwa Ifakara
Halmashauri ya Mji Ifakara imeungana na Watanzania wengine kusherehekea Siku ya Kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania January 27,2024.
Uongozi wa Halmashauri hiyo umesherehekea kwa kufanya haya;
Upandaji Miti katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Ifakara,Eneo la Mahaka ya Mwanzo ya Wilaya ya Kilombero, katika eneo tengwa la Kituo kipya cha Polisi Ifakara na katika Kituo cha Afya Mang'ula
Shule ya Sekondari ya Wasichana Ifakara



Sambamba na hayo Bonanza la michezo limefanyika katika uwanja wa Bethlehem ambapo michezo na Burudani mbalimbali zimefanyika ikiwemo kuwepo kwa Wasanii Wakongwe wa Muziki wa Bongo flavour
