• Nukuu ya Ukaribisho
  • Maswali ya mara kwa mara
  • Mawasiliano Yetu
Ifakara Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Mji Ifakara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Taswira
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Biashara
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Manunuzi & Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
  • Uwekezaji
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Kapu
    • Utamaduni,Sanaa & Michezo
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos

HALMASHAURI YA MJI IFAKARA YAENDELEA NA UTAMBUZI WA KAYA MASKINI

Posted on: January 7th, 2026

HALMASHAURI  YA MJI IFAKARA YAENDELEA NA ZOEZI LA UTAMBUZI WA KAYA MASKINI


Na: Jacqueline Jerome - Ifakara TC, Habari


Mikutano ya wananchi imefanyika katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Mji Ifakara kwa lengo la kutambua na kuorodhesha Kaya zenye hali duni sana ambapo inajumuisha Kaya maskini pamoja na Kaya zilizo kwenye hatari ya kuathiriwa na mabadiliko ya hali ya hewa kama vile mafuriko na ukame ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Serikali wa kuwatambua wananchi wanaohitaji msaada wa kijamii na kiuchumi.


Lengo la zoezi hili si kuandika majina ya kaya tu bali ni kusaidia Serikali iwe na taarifa sahihi zitakazoiwezesha kusaidia wananchi kwa haraka na kwa ufanisi pale kunapotokea dharura au wakati wa kutekeleza programu za kijamii.


Katika mikutano hiyo, viongozi wa Halmashauri kwa kushirikiana na viongozi wa  Serikali za mitaa na Kamati husika, waliwaeleza wananchi vigezo vinavyotumika katika utambuzi wa Kaya maskini ili kuhakikisha zoezi hilo linafanyika kwa uwazi, haki na ushirikishwaji wa jamii, Miongoni mwa vigezo vilivyobainishwa ni pamoja na Kaya zenye kipato cha chini sana zisizo na uhakika wa kumudu mahitaji ya msingi ya maisha kama chakula, mavazi na makazi. Vigezo vingine ni Kaya zisizoweza kumudu au zisizo na uhakika wa kupata angalau milo kamili miwili kwa siku, Kaya zinazoishi katika makazi duni kutokana na kipato kidogo pamoja na Kaya zenye utegemezi mkubwa.


Aidha, Kaya zenye watoto wa umri wa kwenda shule lakini hawajaandikishwa shuleni au wameacha shule kutokana na kukosa mahitaji muhimu ya shule kama sare, madaftari na chakula nazo zimezingatiwa. Vilevile, Kaya zenye watoto wanaoshindwa kupata huduma za afya au kuhudhuria kliniki kwa kukosa uwezo wa kifedha, pamoja na Kaya zinazohudumia watoto wenye uhitaji maalum wa mahitaji muhimu kama makazi, mavazi, chakula, elimu na huduma za afya, zimeorodheshwa kama sehemu ya vigezo vya utambuzi.


Hata hivyo viongozi wa Halmashauri ya Kijiji /mtaa/shehia,kamati za jamii Viongozi wa dini waajiriwa,viongozi wa vyama,wastaafu wanaopokea pensheni hawaruhusiwi kuwa miongoni mwa kaya maskini.

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA KUPIGA KURA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA KITUO TOFAUTI NA KITUO ALICHOJIANDIKISHA

    read more
  • TANGAZO LA ULIPAJI WA ADA NA USHURU KWA WANANCHI, WAFANYABIASHARA NA TAASISI MBALIMBALI IFAKARA MJI

    read more
  • View More

Habari Mpya

  • MKURUGENZI HALMASHAURI YA MJI IFAKARA AKAGUA MWITIKIO WA WANAFUNZI KURIPOTI SHULENI
  • KAMISHNA WA OPERESHENI NA MAFUNZO AKAGUA KITUO KIPYA CHA POLISI KIBAONI ,IFAKARA
  • KAYA MASKINI ZILIZO TAMBULIWA ZAINGIZWA KWENYE MFUMO ILI KUWEZESHA SERIKALI KUTOA HUDUMA KWA HARAKA NA KWA UFANISI
  • HALMASHAURI YA MJI IFAKARA YAENDELEA NA UTAMBUZI WA KAYA MASKINI
  • MADIWANI WILAYA YA KILOMBERO WATAKIWA KUIBUA NA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA KATA
  • More

Mawasiliano Yetu

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Ifakara
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Simu ya Mkononi: -

Kurasa za Haraka

  • CHF
  • Ramani ya halmashauri ya mji wa Ifakara
  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2024
  • BOFYA HAPA KUOMBA KITAMBULISHO CHA WAJASILIAMALI WADOGO
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2024

Kurasa Mfanano

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya utumishi wa uma
  • Tovuti ya mkoa wa Morogoro
  • Tovuti ya Ajira Tanzania

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya Uhifadhi
  • Maswali ya mara kwa mara
  • Ramani