• Nukuu ya Ukaribisho
  • Maswali ya mara kwa mara
  • Mawasiliano Yetu
Ifakara Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Mji Ifakara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Taswira
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Biashara
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Manunuzi & Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Hatua
    • Ripoti
  • Uwekezaji
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Kapu
    • Utamaduni,Sanaa & Michezo
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos

MADIWANI WILAYA YA KILOMBERO WATAKIWA KUIBUA NA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA KATA

Posted on: January 6th, 2026

MADIWANI WILAYA YA KILOMBERO WATAKIWA KUIBUA NA KUSIMAMIA MIRADI  YA MAENDELEO KATIKA KATA ZAO


Na: Nuru Mangalili- Ifakara TC ,Habari


Hayo yamesemwa  Jumanne tarehe 6 /1/2026 na Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Wakili Dunstan Kyobya wakati akifungua Mafunzo Elekezi ya Kuwajengea uwezo Madiwani wa Wilaya ya Kilombero Halmashauri ya Mji Ifakara na Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba yanayofanyika Katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mlimba uliopo Ifakara .


Mhe. Kyobya aliwataka kila Diwani katika Kata yake ahakikishe  anakwenda kusimamia Miradi ya Maendeleo, Mapato, Mikopo ya Asilimia Kumi, Uhifadhi wa Mazingira,  Vyanzo vya Maji, Kutatua Kero za Wananchi,Miundo Mbinu ya Barabara, Mirathi , Maadili na Talaka ,  ulinzi na usalama katika Maeneo yao Ili kuhakikisha Wilaya ya Kilombero inasonga Mbele na kuleta tabasamu kwa Wananchi  wa Kilombero kama ilivyo adhma ya Mhe . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kila mwananchi anapata tabasamu .


Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Bi. Pilly Kitwana aliwapongeza Waheshimiwa Madiwani kwa Mafunzo hayo na kuahidi kuwapa Ushirikiano  katika Utekelezaji wa Majukumu yao ya kila siku Ili kuhakikisha Halmashauri ya Mji Ifakara inasonga Mbele na Kero za Wananchi kutatuliwa kwa wakati .


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba  Mhe. Martha Daniel Mkula alishukuru kwa Mafunzo madiwani na kuahidi kwenda Kutekeleza kwa Ufanisi Yale yote watakayofundishwa na  kuhakikisha wanakwenda kubuni miradi mipya na  inatekelezeka kwa wakati.


Aidha Mafunzo hayo yalihudhuriwa na  Katibu Tawala  Msaidizi anayeshughulikia Masuala ya Serikali za Mitaa  Mkoa wa Morogoro Bi. Neema Dachi  na Bw. Lucas Charles Malunde kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - OWM - TAMISEMI ambapo waliwasisitiza Madiwani hao Kuzingatia mada wanazofundishwa katika Mafunzo hayo Ili zikalete Ufanisi katika Utendaji wao.


Mafunzo hayo ya siku tatu yalianza tarehe 5 Januari 2026 na yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 7 Januari 2025 . Mafunzo hayo yanatolewa na Wakufunzi  kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo.


Latest Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MPIGA KURA KUPIGA KURA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA KITUO TOFAUTI NA KITUO ALICHOJIANDIKISHA

    read more
  • TANGAZO LA ULIPAJI WA ADA NA USHURU KWA WANANCHI, WAFANYABIASHARA NA TAASISI MBALIMBALI IFAKARA MJI

    read more
  • View More

Habari Mpya

  • MKURUGENZI HALMASHAURI YA MJI IFAKARA AKAGUA MWITIKIO WA WANAFUNZI KURIPOTI SHULENI
  • KAMISHNA WA OPERESHENI NA MAFUNZO AKAGUA KITUO KIPYA CHA POLISI KIBAONI ,IFAKARA
  • KAYA MASKINI ZILIZO TAMBULIWA ZAINGIZWA KWENYE MFUMO ILI KUWEZESHA SERIKALI KUTOA HUDUMA KWA HARAKA NA KWA UFANISI
  • HALMASHAURI YA MJI IFAKARA YAENDELEA NA UTAMBUZI WA KAYA MASKINI
  • MADIWANI WILAYA YA KILOMBERO WATAKIWA KUIBUA NA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA KATA
  • More

Mawasiliano Yetu

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Ifakara
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Simu ya Mkononi: -

Kurasa za Haraka

  • CHF
  • Ramani ya halmashauri ya mji wa Ifakara
  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2024
  • BOFYA HAPA KUOMBA KITAMBULISHO CHA WAJASILIAMALI WADOGO
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2024

Kurasa Mfanano

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Wizara ya Tamisemi
  • Wizara ya utumishi wa uma
  • Tovuti ya mkoa wa Morogoro
  • Tovuti ya Ajira Tanzania

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya Uhifadhi
  • Maswali ya mara kwa mara
  • Ramani