MAFUNZO YA URAIA NA UTAWALA BORA KWA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA WA HALMASHAURI YA MJI IFAKARA, MLIMBA,MALINYI NA ULANGA
Wizara ya Katiba na Sheria leo Jumatano tarehe 18 Disemba imetoa Mafunzo ya Uraia na Utawala Bora kwa Viongozi wa Serikali za Mitaa wa Halmashauri ya Mji Ifakara, Wilaya ya Mlimba, Malinyi na Ulanga.
Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Mlimba uliopo Halmashauri ya Mji Ifakara.
Aidha, Mgeni Rasmi katika Mafunzo hayo alikua Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Wakili Dunstan Kyobya ambapo aliwataka Washiriki wa Mafunzo hayo kuzingatia na kuyafanyia Kazi yale yote watakayofundishwa.