Pichani Hapo juu (kushoto). Ikimuonyesha Afisa Tarafa Bi Hawa Mposi akitoa pongezi kwa walimu wakuu nawaratibu elimu kata kwa jitihada walizo onyesha kwenye matokeo ya darasa la 7 .mapema leoNovemba 7/2018 katika shule ya msingi mapinduzi.
Akizungumza na walimu wakuu, waratibu kata elimu, Afisa Tarafa wa mji ifakara ambaye ndie mgeni rasmi katika kikao hicho cha kujua tasmini ya ufaulu katika mtiani wa darasa la saba mwaka huu 2018 na kujiwekea malengo kwa mwaka 2019, Bi Hawa mposi amepongeza walimu washule zote za msingi katika Halmashauri ya Mji Ifakara kwa matokeo mazuri ya mtiani kwa mwaka 2018.
Bi Hawa amesisitiza juu ya walimu kuendelea kufanya kazi kwa wiledi nakuto kiuka taratibu za kazi kwani mmeonyesha juhudi kubwa ya kutokuiba matokeo kwani kunashule ambazo tayari zina sifahiyo kwahivyo muendelee kufanya kazi kwa kufuata maadili ya kazi yenu nguvukubwa na ujuzi wenu utasaidia kupandisha ufaulu katika Halmashauri ya mji Ifakara.
Hatahivyo Afisa Elimu msingi Bi Mariam Nnauye amesema kuwa anashukuru kwa mafanikio yaliyo patikana kwa mtihani wa darasa la saba kwa mwaka 2018 nimazuri . huku akisisitiza kuwa kazi iliyopo mbeleni ni kubwa zaidi ili kutoka katika nafasi ya tano katika Halmashauri ya Mji Ifakara jitihada zitumike zaidi.
“Natarajia kuona mafanikio kwenye mtihani wa darasa la 4 kwa mwaka huu wa 2018 kwani kwajitihada mtakazo zionyesha watafanya vizuiri, lakini pia msingoje kusifiwa jueni huu ni wajibu katika kazi ya ufundishaji kwa waalimu wote hapa nchini.” Alisema afisa elimu msingi mwalimu Mariam Nnauye.
Kwa upande wa waalimu wote wa Shule ya msingi mapinduzi, Ifakara, Kiningina, Lumemo na Kibaoni wamewataka wazazi, walezi kushiriki kwa namna moja au nyingine katika kumjenga mwanafunzia ama mtoto kujali maadili ya shule.
Sambamba na wazazi kuhudhuria vikao pale wanapo hitajika nasikumleta mtoto shuleni na baada ya hapo kuwatelekezea walimu kazi ya kumlea mtoto nijukumu la mwalimu na mzazi ili kumjengea mazingira ya badae na kuongeza ufaulu kwa mwanafunzi.
Hata hivyo imebainika kuwa baadhi ya walezi ama mabibi na wajomba wamekuwa wakizima ndoto za watoto kuendelea kusoma kwa kuwa tegemezi kwa kuwatafutia kipato, badala ya kuwahimiza kwenda shule na kutambuwa kuwa elimu ndiyo ufunguo wa maisha yao hapo baadae.
Baadhi ya walezi wengine kuwaozesha mabinti waliyo chini ya miaka 18, ambao wapo darasa la nne hadi la darasa la sita kinyume na maadili ya mtanzania kupinga ndoa zautotoni.
Kibaoni - Bomani
Sanduku la Barua: 433 Ifakara
Simu ya Mezani: +255 (0)23 - 2934212
Simu ya Mkononi: 0738 223 543
Barua Pepe: td@ifakaratc.go.tz / info@ifakaratc.go.tz
Haki Miliki @2018 Halmashauri ya Mji wa Ifakara . Haki zote zimehifadhiwa